ZUNGUMZA NASI | Tuambie kuhusu mahitaji ya tukio lako kisha tutaandaa pendekezo la kina maalumu kwa ajili yako tu | OMBA PENDEKEZO |
|
Sasa Imefunguliwa Eneo la vikao, mikutano na harusi la Johari Rotana linalotawala ukubwa wa mita za mraba 2,000 na likiwa na teknolojia ya kisasa kabisa ni moja ya maeneo makubwa na ya kisasa kabisa katika Jiji la Dar es Salaam na limeundwa kwa ajili ya kuhudumia matukio ya aina mbalimbali. Bwalo la Almasi lenye ukubwa wa mita za mraba 816 ni bwalo la hotelini kubwa kabisa Tanzania na ni bwalo linaloweza kubadilika sana Jijini linaloweza kuwahudumia hadi wageni 950. Linaweza kutumiwa lote au likagawanywa katika sehemu tofauti na linafaa kwaajili ya matukio mbalimbali kuanzia mikutano, mikusanyiko ya kijamii, sherehe za mashirika na sherehe ndogo za cocktail hadi matukio maalumu, ikiwa ni pamoja na harusi. Vyumba vyote sita vya mikutano vipo kwenye ghorofa moja na vinaweza kupangwa katika miuundo kadhaa tofauti, wakati Suite ya Bibi Harusi inaweza kutumika kama chumba cha wageni Muhimu Sana (VIP) au eneo la maandalizi kwa mikutano mikubwa. Kumbi zote zimekamilika na vifaa vya sauti va video vya kisasa, intaneti ya Fibre Optic, mwanga wa mchana wa asili na mandhari nzuri ya bandari ambayo itawavutia wageni wako. Timu zetu za wataalamu wa kuandaa matukio na kutoa huduma ya chakula watahusika na kila kitu, kuanzia mapambo na mpangilio wa ukumbi hadi menyu zinzotayarishwa kwa upekee. |